Saturday, April 26, 2014

KAMATI za ulinzi mkoani Shinyanga zaazimia kuwashughulikia wanaohujumu miundo mbinu ya mawasiliano.


KAMATI za ulinzi na usalama za halmashauri za wilaya ya shinyanga, kishapu na manispaa ya shinyanga pamoja na jeshi la jadi la sungusungu wameazimia kuwashughulikia watu wanaosadikiwa kuhujumu miundo mbinu ya Barabara, Shirika la umeme nchini, Tanesco, shirika la Reli nchini, TRL na shirika la simu nchini TTCL mkoan humo.
 
Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na viongozi hao pamoja na makamanda wa jeshi la jadi la sungusungu kutoka halmashauri hizo hapo jana baadhi ya viongozi waliowakilisha taasisi hizo na mashirika hayo ya umma, wamesema kutokana na kuendelea kupata hasara, uharibifu wa mali na watu kupoteza maisha, vinayotokana na kuhujimiwa kwa miundombinu hiyo, wameamua kuweka mkakati wa pamoja wa kupambana na wahalifu hao.
 
Wamesema wizi wa miundombinu hiyo ambayo imekuwa ikidaiwa kutumika katika kutengeneza majembe ya kukokotwa na ngombe, plau, pamoja biashara ya vyuma chakavu, imekuwa ikisababisha shughuli mbalimbali za ukuaji wa uchumi na huduma za kijamii kuzorota.
 
A
 

No comments:

Post a Comment