RAISI
wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
amemtumia Salamu za Rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mheshimiwa Perseko Kone
kufuatia vifo vya watu 19 wakiwemo Askari Polisi wanne na Viongozi watatu
wa Kijiji kufuatia ajali ya barabarani iliyosababishwa na basi lililokuwa
likitokea Kigoma kuelekea Dar es Salaam katika Barabara kuu ya Singida -
Dodoma.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Kurugenzi
ya Mawasiliano ya Rais Ikulu jijini Dar es salaam,ajali hiyo ilitokea usiku wa
April 27mwaka huu katika Kijiji cha Utaho, Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida
baada ya basi la Kampuni ya Sumry lenye Nambari ya Usajili T. 799 BTE aina ya
Nissan kuwagonga watu waliokuwa wamekusanyika katika eneo ambapo ajali nyingine
ilikuwa imetokea wakiwa pamoja na Askari Polisi kutoa msaada katika ajali
nyingine iliyokuwa imetokea katika eneo hilo ambapo mwendesha baiskeli
aligongwa na lori na kufariki papo hapo.
Rais Kikwete amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Singida,
Mheshimiwa Perseko Kone kumfikishia Salamu zake za Rambirambi na pole nyingi
kwa watu wote waliopotelewa na ndugu na jamaa zao kutokana na ajali hiyo, na
amewahakikishia wafiwa kuwa yuko pamoja nao katika kuomboleza msiba huo mkubwa.
No comments:
Post a Comment