WAKULIMA wadogo nchini
wameshauriwa kuwa na tabia ya kutembeleana mara kwa mara kwa ajili ya
kubadilishana uzoefu na wakulima wenzao ili waweze kupata mbinu bora za
kilimo.
Rai hiyo imetolewa na maafisa kilimo katika
kijiji cha IBINGU wilaya kilosa mkoani Morogoro wakati wa ziara ya kutembeleana
wakulima wanaotekeleza Mradi wa mabadiliko ya tabia nchi,Kilimo na kupunguza
umasikini katika vijiji vya mradi ambavyo ni Madudumizi,Ilakala,Ibingu na Ulaya
Kibaoni
Afisa kilimo kutoka MVIWATA Bwana Amanzi Amanzi
amesema lengo la ziara hiyo ni kuwasaidia wakulima wabadilike na kulima
kilimo bora chenye kuleta tija kwa kuwa tayari wamefundishwa mbinu
ambazo haziharibu mazingira.
Kwa upande wake Afisa kilimo kutoka Mtandao wa
kijamii wa kuhifadhi misitu MJUMITA Bwana Ernest Jerome amewataka wakulima
kushirikiana katika shughuli za kilimo na ndio maana wameamua kufanya ziara ya
mafunzo ili kufahamiana na kubadilishana ujuzi.
Ziara hiyo imeandaliwa na mtandao wa vikundi
vidogo vya wakulima nchini MVIWATA kwa kushirikiana na Mtandao wa jamii
wa kuhifadhi misitu TANZANIA MJUMITA.
No comments:
Post a Comment