IMEELEZWA kuwa nchi ya Afrika ya
kusini, Uingereza na Canada zilichangia kwa wastani wa zaidi ya asilimia 70 ya
uwekezaji wote kutoka nje kati ya mwaka 2008 na 2011.
Hayo yamebainishwa hivi
karibuni jijini Dar es salaam na wataalamu wa Benki kuu(BOT) Kitengo cha sera
katika mahojiano maalum na mbiu ya maendeleo.
Wameeleza kuwa, Ripoti
ya uwekezaji ya mwaka 2012 utafiti uliofanywa na Benki kuu, , Taasisi ya takwimu nchini (NBS) kuhusu hali ya uwekezaji nchini ilibaini kuwa
nchi hizo ndizo zilizowekeza mitaji toka nchi kwa asilimia kubwa.
Wamesema, kilimo ambacho
kina mchango mkubwa kwenye pato la taifa kiliendelea kuwa na kiwango kidogo cha
uwekezaji toka nje ikilinganishwa na uwekezaji kkwenye shughuli nyingine kama
uchimbaji wa madini na mawe, uzalishaji viwandani, fedha na bima na habari na mawasiliano.
Mbali na hayo wamesema
kuwa faida baada ya kulipa kodi iliongezeka kwa wastani wa asilimia 79.3 kila
mwaka toka mwaka 2009 mpaka mwaka 2011
No comments:
Post a Comment