Wednesday, April 30, 2014

ASILIMIA 95 ya kaya nchini Tanzania inatumia chandarua cha kuzuia mbu



TUKIWA katika wiki ya malaria duniani takwimu toka viashiria  vya ukimwi na malaria  nchini inajuza kuwa miongoni mwa kaya  zote nchini Tanzania,asilimia 95 ya kaya inatumia  chandarua cha kuzuia mbu anayeeneza ugonjwa wa  malaria ambapo asilimia 91 ya kaya nchini wana tumia vyandarua vyenye dawa ya kuuwa mbu.

Taarifa toka wizara ya afya na wadau wa Ukimwi na amalaria kwa vyombo vya habari zinaeleza kuwa hali hiyo imetokana na wizara ya Afya na wadau mbalimbali wa mapmbano dhidi ya malaria kugawa dawa , vyandarua na kutoa elimu ya afya kwa umma katika kila kona ya Tanzania na kutumia vyombo mbalimbali vya habari katika kuelimisha jamii .

Umiliki wa vyandarua katika kaya kwa asilimia tajwa hapo juu ni kiashiria tosha cha mafanikio ya vita ya kupambana na ugonjwa wa malaria
.



No comments:

Post a Comment