SERIKALI imesema itahakikisha inasimamia
na kutatua matatizo ya wafanyakazi pamoja na kudhibiti mianya ya uingizwaji
holela wa bidhaa za nje ya nchi ambazo zinachangia kudidimiza soko la
ndani.
Rai
hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Morogoro Bwana Said Amanzi kwa niaba ya
mkuu wa mkoa wa Morogoro Dr.Joel Nkaya
Bendera
katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi duniani
iliyofanyika kimkoa katika uwanja wa jamhuri mjini Morogoro.
Bwana
Amanzi ameyasema hayo wakati akijibu risala ya wafanyakazi iliyokuwa
ikiiomba serikali kudhibiti bidhaa za nje kuingia nchini ili kutoa nafasi
kwa soko la ndani.
Awali
akisoma risala ya wafanyakazi mratibu wa sherehe hizo Charles Luvunzo
amewata wafanyakazi kuungana ili kupatiwa mahitaji muhimu ikiwemo
kupigania stahiki zao kwa kuhifadhiwa fedha katika mifuko ya jamii.
No comments:
Post a Comment