Thursday, May 1, 2014

SERIKALI yashauriwa kutengeneza miundo mbinu ya elimu ili kuwawezesha walemavu kusoma



SERIKALI imeshauriwa kusaidia kutengeneza miundombinu rafiki katika maeneo mbalimbali ikiwemo shuleni,itakayowawezesha watoto wenye ulemavu kupata elimu kwa urahisi .

Aidha imeshauriwa kuhakikisha inatekeleza sera ya Taifa inayoelekeza elimu bure kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano kwa kujumuisha pia watoto wenye ulemavu.

Ushauri huo umetolewa na Meneja  Programu ya Elimu kutoka Shirika lisilo la kiserikali  la CCBRT linalotoa huduma kwa Watu wenye ulemavu, wakati wa ziara ya wanahabari kwenye Kituo cha watoto wenye ulemavu kilichopo Manzese wilayani Kinondoni jijini Dar es salaam, ambapo tangu mradi wa kusaidia watoto mashuleni uanze mwaka 2005 zaidi ya watoto 2000 wamenufaika, ingawa tatizo kubwa ni kutokuwepo kwa mazingira rafiki kwa watoto hao.

No comments:

Post a Comment