ZAIDI ya hekari 400 za mashamba ya miti zinateketezwa kila mwaka kwaajili
ya kutengeneza mkaa, Imeelezwa.
Hayo
yamebainishwa hivi karibuni jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa utafiti na
matumizi ya nchi toka mamlaka ya hali ya hewa nchini Dk Ladislaus Chang’a wakati
akiongea na wanahabari kuhusu mabadiliko ya hali ya nchi na athari zake.
Dk
Chang’a amefafanua kuwa viashiria vya madbadiliko ya hali ya hewa nchini ni
pamoja na mafuriko kila sehemu kutokana na mvua chache zinazoendelea kunyesha,ongezeko
la joto,mabadiliko ya msimu wa mvua,kuyeyuka kwa barafu mlima wa Kilimanjaro na
ongezeko la ugonjwa wa malaria hata katika mikoa ambayo miaka ya nyuma ugonjwa
huo halikuwa tishio.
Amesema
mkoa wa Dar es salaam pekee huwa yanatumika magunia sitini elfu ya mkaa kwa siku kwaajili ya matumizi
mbalimbali.
.
No comments:
Post a Comment