Friday, May 2, 2014

WAZIRI wa kazi na ajiri ameyataka mabaraza ya kazi kwa kuangalia tija badala ya kulalamikia maslahi duni



WAZIRI wa kazi na ajira Mheshimiwa Gaudensia Kabaka amesema pamoja na mabaraza ya kazi kuangalia na kusimamia haki za wafanyakazi ni vema pia yakaangalia tija ya mfanyakazi katika eneo lake la  kazi ili kwenda sambasamba na madai yao.

Waziri Kabaka ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam,wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo ambapo amesema wizara yake imejipanga kuimarisha na kuboresha ofisi za kazi mikoani kwa kuziongezea bajeti  mwaka huu jambo litakalosaidia katika kuboresha utendaji kazi ikiwemo kuwafikia wafanyakazi walio pembezoni.

Waziri Kabaka amesema mara nyingi kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wafanyakazi hususani wa sekta binafsi ambao wamekuwa hawaangalii utendaji wao kama unamnufaisha pia mwajiri hivyo kuibua migogoro sehemu za kazi.

Aidha ameyataka makampuni yote yanayojiuhusisha na uwakala wa huduma za ajira nchi kujisajili ili kubaini yale yanayoendesha shughuli hizo kinyume cha sheria ambapo amebainisha kuwa katika sheria za kazi zilizopo sasa hakuna suala la kibarua katika maeneo ya kazi bali kuna mkataba wa muda mfupi, mrefu na wa kudumu.

No comments:

Post a Comment