Friday, May 2, 2014

WAUMINI wa kanisa la Sabato wamewataka wajumbe wa bunge maalum la katika kuondoa itikadi zao za kisiasa ili kupata katiba yenye manufaa kwa Taifa



WAUMINI wa kanisa la wa Adventista wasabato wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro,wamewataka  wajumbe wa Bunge Maalum la katiba kuweka itikadi zao  za kisiasa pembeni pindi watakapo rejea Bungeni mjini Dodoma, ili kuweza kupata katiba mpya itakayokidhi matakwa ya Watanzania ,badala ya kuendeleza malumbano yasiyo  na maslahi kwa Taifa .

Waumini hao wametoakauli hiyo jana baada ya ibada maalumu ya kuwaombea vijana wa kanisa hilo, walio hitimu mafunzo ya ualimu  ngazi ya stashahada , katika chuo cha ualimu Greenbird   kilichopo wilayani Mwanga  mkoani humo.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya waumini  wamesema, wamesikitishwa na  malumbano na kejeli  zilizokuwa zikifanywa  na  baadhi ya wajumbe wa bunge la katiba mjini Dodoma ,   hivyo  wabadilike na watumie muda uliobakia kurejesha busara zao  kwa  kukaa pamoja, ili ipatikane katiba bora kwa manufaa ya Taifa.

No comments:

Post a Comment