Wednesday, April 16, 2014

WAKAZI wa mkoa wa Ruvuma waipongeza Sumatra



BAADHI ya Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma wameisifu Mamlaka ya Usafiri wa nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kwa kuweza kusimamia safari za Mabasi na kufanikisha kupanga safari katika sehemu ambazo zilikuwa na kero ya usafiri kwa Wananchi wa Mkoa huo.
                       
Akizungumza kwa niaba ya Wasafiri wenzake katika Kituo Kikuu cha Mabasi Songea mapema leo ,mmoja ya wakazi wa  mji wa  Songea  Bwana Mohamedi Chichi,amesema katika Changamoto zilizokuwa zinawakabili Wananchi wa Mkoa wa Ruvuma ni kukosa Usafiri wa Songea – Dodoma, Songea – Mwanza na Songea – Mbamba Bay ambapo kwa sasa  Njia zote hizo zimefunguka na ameishukuru Serikali kwa kuweza kutatua changamoto hiyo.

Nae Afisa Mfawidhi wa SUMATRA Mkoa wa Ruvuma bwana Denis Daudi amesema Mkoa wa Ruvuma una changamoto nyingi za usafiri, ikiwemo usafiri wa Songea – Mkenda –njia ambayo inaunganisha Nchi ya Msumbiji na Tanzania pamoja na ile ya Songea  Tunduru ambayo bado inahitaji Usafiri wa uhakika.

No comments:

Post a Comment