ZAIDI ya kaya 424 zilizopo Manispaa ya Morogoro zenye
jumla ya watu 2120 zimeathirika na mafuriko hayo na zinahitaji msaada wa
kibinaadamu ambapo tayari mifuko 200 ya unga wa sembe imekabidhwa kwenye
ofisi ya mkuu wa wilaya Morogoro kutoka ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Morogoro
mjini,mheshimiwa Abdul azizi Mohamed Abood yenye thamani ya shilingi milioni 4
na laki 6 kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yanayosababishwa na mvua
hizo
Kutokana na hali hiyo Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt Joel Bendera
amewataka wananchi waliojenga katika mikondo ya maji kuondoka mara moja ili
kuepuka madhara yanayotokana na mafuriko.
Kauli hiyo ameitoa hivi karibuni wakati kamati ya ulinzi na
usalama ya mkoa huo ilipotembelea na kuangalia maeneo ya Manispaa ya Morogoro
yaliyoathirika na mafuriko yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini
Dkt Bendera amesema, Serikali ya mkoa wa Morogoro inaendelea
kufanya tathimini ya watu walioathirika na mafuriko ili iweze kuangali namna ya
kuwasaidia.
No comments:
Post a Comment