Sunday, April 20, 2014

WANANCHI wilayani Kondoa wahimizwa kutumia fursa ili kujiletea maendeleo



WANANCHI  wa vijiji 57 vya wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma, wamehimizwa kutumia fursa iliyojitokeza ya kupata umeme katika maeneo yao, ili waweze kujiletea maendeleo na kukuza uchumi wao.

Wito huo umetolewa hivi karibuni na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, katika kijiji cha Itololo, wilayani Kondoa, wakati alipokuwa akikagua utekelezaji wa mradi wa umeme vijijini,ambapo kwa mkoa wa Dodoma utagharimu shilingi bilioni 43.9.

Naye, Mbunge wa Kondoa Kaskazini, Bi Zabein Mhita akizungumza kwa niaba ya wananchi wa vijiji vitakavyofikiwa na mradi huo wa umeme, amesema mwamko ni mkubwa kutoka kwa wananchi hao, kwa kuwa wanatambua umuhimu wa umeme katika maendeleo yao.

 Hatua iliyofikiwa kwa sasa ni upelekaji wa nguzo za usimikaji wa umeme katika vijiji hivyo, na inatarajiwa kuwa pindi umeme huo utakapowashwa utasaidia kuongeza thamani ya mazao ya wananchi wa vijiji hivyo kwa kuyasindika, na hata huduma za jamii kama shule na hospitali, kuwa bora zaidi.











No comments:

Post a Comment