Sunday, April 20, 2014

KAMATI ya fedha Manispaa ya Morogoro yatembelea miradi ya maendeleo



KAMATI ya Fedha na uongozi ya manispaa ya Morogoro imefanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo hospitali ya wilaya ambayo imeanza kujengwa katika kata ya Mkundi Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo iliyofanyika jana Meya wa Manispaa ya Morogoro bwana Amir Nondo amesema ujenzi huo umefikia hatua nzuri na wanasubiri kapata fedha awamu ya pili ili waweze kukamilisha jengo hilo ambapo ameishukuru serikali kwa kuwapatia fedha.

Bwana Nondo amefafanua kuwa wamejenga hospitali hiyo ya wilaya katika kata ya Mkundi kutokana na wakazi wa kihonda, Mkundi na maeneo mengine kuwa mbali na huduma ya afya.
Ujenzi wa hospitali hiyo unaotarajia kukamilika April 26 mwaka huu hadi sasa umegharimu kiasi cha shilingi milioni mia tano na elfu themanini na tano.






No comments:

Post a Comment