TUME ya kurekebisha sheria nchini, imekabidhi
taarifa ya mapitio ya mfumo wa utatuzi wa migogoro ya aridhi nchini, kwa waziri
wa Katiba na Sheria, Dk. Asha Rose Migiro.
Akikabidhi taarifa hiyo, Mwenyekiti wa
Tume ya Kurekebisha Sheria Nchini Jaji Aloysius Mujuluzi, amesema tume yake
imeonelea kuangalia eneo hilo ambalo limekuwa linalalamikiwa na wananchi, ili kutoa mapendekezo ya namna
sheria hiyo inavyoweza kurekebishwa, kuondoa kasoro za kisheria na kutekelezwa
kwa ubora na mafanikio zaidi.
Akipokea taarifa hiyo, Waziri wa Katiba na
Sheria Dk. Migiro amepongeza juhudi zinazofanywa na tume kuhakikisha sheria
zina kwenda na wakati, na zile zenye kasoro zinarekebishwa, na hivyo ameahidi
wizara yake kuchukua kwa uzito unaostahili mapendekezo yaliyotolewa,ambapo
akatoa rai kwa watendaji.
Mapitio ya mfumo
wa utatuzi wa migogoro ya aridhi, yanafanywa baada ya miaka kumi toka mfumo huo
uanzishwe nchini, kupitia mahakama maalum za ardhi, ili kuona na kupima ufanisi
wa taasisi hizo juu ya dhamana kubwa ya kutatua migogoro ya ardhi, huku
ikizingatiwa kuwa aridhi ndio msingi wa maisha ya mwanadamu.
No comments:
Post a Comment