Saturday, May 17, 2014

WATANZANIA wakumbushwa umuhimu wa kutunza na kuhifadhi mazingira



WATANZANIA  wamekumbushwa kutambua umuhimu wa kutunza na kuhifadhi mazingira ikiwa ni pamoja na kuangalia namna ya kutopoteza wanyama kwa kuwa ni miongoni mwa rasilimali zinazoliingizia taifa mapato kwa kiasi kikubwa.

Akizunguma na baadhi ya Walimu wa Shule za Sekondari za Mkoa wa Dar es salaam, ambao walikuwa wakipatiwa elimu juu ya kuwawezesha vijana mashuleni kujua faida za utalii, uhifadhi wa mzingira na kutambua fursa zilizopo katika sekta ya utalii, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Wanyamapori kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. HERMAN KARARYO, amesema licha ya mabadiliko ya Tabia nchi kuleta matatizo, lakini wananchi wenyewe wamekuwa wakisababisha uharibifu wa mazingira.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Maendeleo ya Wanawake , Vijana na Mazingira AWEIDA Halima Mamuya amebainisha kuwa wakati umefika sasa wa kuwawezesha wanafunzi mashuleni kutambua umuhimu wa kutunza, kuhifadhi na kujua fursa za utalii tangu wakiwa wadogo.

Mkutano huo umeandaliwa na Chama cha Maendeleo ya Wanawake , Vijana na Mazingira AWEIDA kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Usafiri na Utalii Afrika Mashariki GTTP.
 --------------------------------------------------------------------------------











No comments:

Post a Comment