Sunday, May 18, 2014

WADAI wa DECI wilayani Kilosa waikumbusha serikali kutekeleza ahadi yake ya kuwarejesha wahanga fedha zao


WALIOKUWA wanachama wa chama cha kupanda  na kuvuna DECI Wilayani Kilosa wameiomba serikali iwarejeshee pesa zao kama ilivyowaahidi au itoe tamko lolote juu ya pesa zao ili wafahamu kinachoendelea.

Wakizungumza na Mwandishi wa Habari Kilosa baadhi ya wanachama hao wamesema serikali  imekaa kimya kwa muda mrefu kitu ambacho kinawapa wasiwasi wa kurejeshewa pesa zao kama serikali ilivyowaahidi.

Mmoja wa wanachama hao Nassoro Machengo ambaye alipanda zaidi ya milioni moja amesema baada ya serikali kuthibitisha na kuifungia Taasisi hiyo na kuipeleka mahakamani ili ahidi kurejesha pesa kwa wananchi waliotoa fedha zao DECI wenye ushahidi wa vielelezo mara tu kesi hiyo itakapokamilika .
Ni miaka 7 sasa tangu Taasisi ya kifedha ya DECI iliyokuwa ikijiendesha katika utaratibu wa kupanda na kuvuna pesa ambapo wananchi mbalimbali waliwekeza pesa kwa  lengo la kuvuna pesa zaidi , lakini Taasisi hiyo ilikuwa ikiendeshwa kinyume na taratibu za kisheria hivyo serikali ilisimamisha kufanya shughuli hizo huku ikiwa imekusanya  mabilioni ya watanzania.

No comments:

Post a Comment