Sunday, May 18, 2014

SERIKALI imeombwa kuwajengea uwezo walemavu ili waweze kujiajiri na kuepuka tabia yakuwa tegemezi


CHAMA cha Watu wenye ulemavu Mkoa wa Mara CHAWATA kimeiomba Serikali kushirikishwa katika Masuala mbalimbali yanayowahusu ikiwemo kujengewa uwezo ili kujitegemea na kuondoa dhana ya watu wenye ulemavu ni tegemezi.

Wakiongea katika Jukwaa la Majadiliano kuhusu ujumuishwaji na utetezi wa Mahitaji na haki za watu wenye ulemavu wa viungo, baadhi ya watu wenye ulemavu mkoani Mara wamesema kuwa wamekuwa wakitengwa katika mambo mbalimbali ikiwemo kutokuwepo kwa miundombinu rafiki katika baadhi ya ofisi mkoani humo na kuwa  kikwazo katika kupata huduma wanazozihitaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CHAWATA Mkoa wa Mara Bw Yohana Magai amesema kuwa ni vigumu masuala ya watu wenye ulemavu kujadiliwa na watu wasiokuwa na ulemavu .

CHAWATA mkoa wa Mara kimeweza kufanya Majadiliano hayo katika Jukwaa hilo kwa ufadhili wa Taasisi ya The foundation For Civil Society ya jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment