WIZARA ya Utalii nchini, imeombwa kuweka
utaratibu mzuri wa kuwawezesha watalii wa ndani kutembelea vivutio vilivyopo
nchini bila kupitia katika makampuni ya kupandisha watalii na badala yake
waruhusu vikundi binafsi ili kuleta muamko kwa watanzania wengi
kuvitembelea vivutio hivyo.
Wakiongea
baada ya kutembelea uwanda wa kilele cha mshira katika mlima Kilimanjaro,hivi
karibuni baadhi ya watalii wa ndani wamesema, watanzania hawana utamaduni wa
kuvitebele vivutio vya nchi yao kutokana na kukosekana kwa hamasa, pia urasimu
wa kuvitembele vivutio hivyo.
Wamesema
ili kuleta muamko kwa watanzania ,wanaiomba wizara husika kuweka viwango
ambavyo wananchi wa hali ya chini wanaweza kuvimudu,
pia kutoa elimu na hamasa kuanzia shule za msingi ili jamii iweze kujengwa
katika misingi ya kuvitambua na kuvithamini vivutio vyao.
No comments:
Post a Comment