Sunday, May 18, 2014

MANISPAA ya Morogoro yaanza zoezi la kutoa chanjo ya kichaa cha mbwa kwa lengo la kutokomeza ugonjwa huo


HALMASHAURI ya manispaa ya Morogoro imeaanza zoezi la kutoa chanjo ya kichaa cha  mbwa lengo likiwa ni kutokomeza ugonjwa  huo.

Afisa mifugo wa kata ya Kichangani Bi Mary Shayo amesema chanjo hiyo inatolewa kwa mwaka mara moja na kuwahamasisha  wakazi wa eneo hilo kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi hilo.

Aidha bi Shayo amesema kuwa malengo yao ni kuchanja mbwa wapatao mia mbili hivyo wananchi wanatakiwa kutambua umuhimu wa kupeleka mbwa pamoja na paka ili waweze kupatiwa chanjo hiyo.

Tatizo  la ugonjwa wa kichaa cha mbwa linaongezeka siku hadi siku hivyo elimu zaidi inatakiwa kutolewa kwa wananachi ili kupunguza tatizo la ugonjwa huo.

No comments:

Post a Comment