MAKTABA ya wilaya
ya Kilosa ,mkoani Morogoro inakabiliwa na changamoto mbalimbali hali
inayopelekea maktaba hiyo kushindwa kujiendesha vizuri.
Hayo yameelezwa jana na mkutubi wa
maktaba hiyo James Mgunga wakati akiongea na mwandishi wetu ofisi kwake na
kuzitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na uchakavu wa jengo la
maktaba,upungufu wa vitabu vya kiada na uhaba wa wasomaji.
Mgunga amesema kuwa changamoto hizo
zinapelekea wasomaji kushindwa kujtokeza kwa wingi kwenda kujisomea katika
maktaba hiyo hali inayochangia maktaba hiyo
kushindwa kujiendesha kwani inategemea mapato kutoka kwa wasomaji.
Kutokana na hali hiyo mkutubi huyo amewaomba wafadhili na wadau mbalimbali wa maendeleo
wajitokeze kukarabati jengo la maktaba ili liwe katika hali nzuri kwani
iliyopo sasa ni mbaya kwani jengo limechakaa sana.
No comments:
Post a Comment