Monday, May 19, 2014

WADAU wa zao la kahawa wametakiwa kufanya tathmini ya matatizo yanayowakabili



WADAU wa kahawa mkoani Kilimanjaro wametakiwa kufanya tathimini ya kina kuhusu matatizo yanayo kikabili kilimo cha zao la kahawa ,kisha kuyatafutia ufumbuzi ili zao hilo liweze kulimwa kwa wingi na mkoa huo uweze kukuza uchumi wake na Taifa kwa ujumla

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Bw Leonidas Gama, wakati akifungua warsha ya wadau wa  kilimo cha zao la kahawa iliyofanyika mjini Moshi, ambapo amesema mkoa huo uko nyuma kiuchumi ,kutokana na baadhi ya wakulima kubadili    kilimo cha kahawa ,na kuanza kulima mazao ya aina nyingine.  

Bw Gama amezitaja sababu  za kushuka kwa kilimo hicho,ni pamoja na wakulima kutozingatia kanuni za kilimo bora  ,ufinyu wa ardhi kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya watu , vijana kukimbilia mijini na kuwaachia wazee shughuli  za kilimo ,pamoja na mabadiliko ya tabianchi.


Baadhi ya wakulima wa kahawa waliohudhuria katika semina hiyo ,wameiomba serikali iwapatie wakulima hususani vijana elimu ya kilimo bora  pamoja na pembejeo ,ili vijana hao wasikimblie mijini na kuwaachia wazee kazi za mashambani


No comments:

Post a Comment