Monday, May 19, 2014

WAFANYABIASHARA wametakiwa kutoanika juani bidhaa za vyakula ili kuepusha madhara kwa mlaji



WAFANYABIASHARA  wa maduka ya jumla na rejareja wilayani Kilosa wametakiwa kucha tabia ya kuanika juani biashara za vyakula ili kuepuka madhara ya kiafya.  

Wito huo umetolewa na afisa afya upande wa chakula na vipodozi[TFDA]wilayani Kilosa  Bwana  Fransis Jacob ofisini kwake mapema leo  wakati akiongea na wanahabari kuhusu  majukumu na kazi za mamlaka ya chakula na madawa nchini(TFDA)

Jacob amesema kuanika bidhaa juani kunaharakisha bidhaa kuisha muda wake hivyo amewataka wauzaji wa bidhaa kuacha tabia hiyo.

Amesema lengo la mamlaka ya chakula dawa na vipodozi TFDA ni kulinda afya ya wananchi na jamii kwa ujumla kwa kuzuia athari  ambazo zinaweza kujitokeza kwa mlaji.

No comments:

Post a Comment