Monday, May 19, 2014

SERIKALI imesena ujenzi wa barabara ya kidatu -Ifakara mpaka Mlimba , wilayani Kilombero unaendelea



SERIKALI  imesema inaendelea na ujenzi wa barabara ya Kidatu- Ifakara hadi Mlimba wilayani Kilombero mkoani Morogoro ili  barabara hizo ziweza kupitika kwa muda wote ambapo kwa  sasa    zinafanyiwa upembuzi yakinifu ili kuweza kuanza ujenzi wake mara moja.

Hayo yamesemwa leo Bungeni Mjini Dodoma  na Naibu waziri wa Ujenzi mhandisi  Gerson  Lwenge  alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Abdul  Mteketa aliyetaka kujua ni lini barabara za jimbo lake zitakamilika kujengwa ili ziweze kupitika kwa mwaka mzima kuliko ilivyo  hivi sasa ambapo barabara nyingi hazipitiki na kupelekea adha kwa wakazi wa eneo hilo

Wakati huohuo Serikali imetupiwa lawama kwa kushindwa kusimamia elimu nchini na badala yake serikali kupitia wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi inasaidia kuididimiza elimu kutokana na  mipango yake isiyo zingatia taaluma na umakini kama ilivyojitokeza   kwenye ufaulu wa mitihani ya kidato cha nne mwaka jana kwa kuwa  na sifuri nyingi  na kuongeza madaraja ya ufaulu yasio kuwa na tija.

Lawama hizo zimetolewa na msemaji wa kambi rasmi ya upinzani bungeni Mheshimiwa Suzan Limo wakati akiwasilisha maoni ya kambi hiyo na  kusema, serikali inakwepa wajibu wake katika kuendeleza elimu nchini badala yake inasaidia kushusha elimu kwa kutowajibika ipasavyo

No comments:

Post a Comment