Friday, May 16, 2014

WIZARA ya afya na ustawi wa jamii yaombwa kufikisha elimu ya homa ya dengue vijijini


WANANCHI  wa wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro wameiomba wizara ya afya na ustawi jamii kupitia wataalamu wa Afya wa halmashauri kuaandaa mpango maalum wa kutoa elimu kwa wananchi juu ya ugonjwa wa homa ya Dengue.

Wakiongea na wanahabari mjini Ifakara mapema jana ,wananchi hao wamesema kuwa, watu wengi hawana ufahamu wa kutosha juu ya ugonjwa wa dengue hivyo ni vyema serikali ikachukua tahadahri kwa kuhakikisha kuwa wananchi wanapatiwa elimu ya kutosha juu ya ugonjwa huo.

Mazingira ya Ifakara yanafanana na  yale ya  jiji la Dar es salaam, hivyo huenda ugonjwa huo ukaingia wilayani kwetu, sasa wizara ni lazima ihakikishe inatuapatia wananchi wake elimu ya kutosha , walisema wakzi hao wa Ifakara , Kilombero

No comments:

Post a Comment