Friday, May 16, 2014

WIZARA ya maliasili na utalii yaingiza shilingi milioni 931,611,239 kutokana na biashara ya mazao ya misitu


SERIKALI imeingiza kiasi cha shilingi za kitanzania zipatazo 931,611,239 kwa mwaka 2013/2014 zilizokusanywa kutokana na udhibiti wa biashara ya mazao  ya misitu.

Hayo yamebainishwa juzi na waziri wa Maliasili na  Utaliii Mheshimiwa Lazaro Nyarandu alipokuwa akiwasilisha bajetio ya wizara hiyobungeni mjini Dodoma

Ameeleza kuwa  doria hizo zilifanyika nchi nzima jumla ya watuhumiwa 263 wa biashara hiyo walikamatwa kati yao 72 walifungwa na 176 walilipa faini ,watatu waliachiwa huru na 12 hukumu hazijatolewa.

Mbali na hayo jumla ya vipande 1,000,015vya mbao,mkaa mifuko 48,235 na magogo 8,520 yamekamatwa

No comments:

Post a Comment