Tuesday, May 13, 2014

BODI ya maji nchini Malawi yaanzisha utaratibu wa ujumbe wa simu kwa wateja wake ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa muhimu



BODI ya maji katika mji wa Branytre nchini Malawi  umeanzisha huduma ya ujumbe mfupi kwa njia ya simu ya kiganjani ili kurahisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali kwa wateja wake.
Afisa wa bodi anayeshughulikia masuala ya umma Bi Priscilla Mateyu ameeleza hay oleo kupitia taarifa yake kwa umma na vyombo vya habari nchini humo, kuwa kupitia taarifa hiyo mteja wa maji atapata kufahamu ankra za malipo ya uzilizopita na za sasa , taarifa za kukatika kwa maji na huduma za maji zinazotolewa na bodi hiyo.
Bi mateyu amesema kuwa .utafiti umebaini kuwa, wananchi wengi nchini humo hawana uwezo wa kupata taarifa kupitia redio, runinga na hata magazeti, hivyo huduma hiyo itaondokea kero kwa wateja wao.

 

No comments:

Post a Comment