Tuesday, May 13, 2014

IDADI ya wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu yaongezeka



WAZAZI na walezi nchini wameonywa kutowageuza wanafunzi kuwa “yaya’ wa kuwalea watoto ili kupunguza kasi ya wanafunzi wasiojua kusoma , kuandika na kuhesabu .
Rai hiyo imetolewa na wadau wa elimu wilaya ya Katavi, mkoani Katavi katika mahojiano maalum wakati wakati wakitahmini hali ya elimu wilayani humo.

Wameeleza kuwa, tafiti za elimu zimebaini kuwa , wanafunzi wengi hawahudhurii darasani kutokana na kupangiwa majukumu ya kulea wadogo zao nyumbani na hivyo ku uwanyuma kitaaluma.

Wilaya ya Katavi mkoani Katavi ina jumla ya wanafunzi 1500 wasiojua kusoma, kuandika na kuhesabu (kkk), ambapo  tafiti hizo zimebaini kuwa wilaya ya Mwanga ,mkoani Kilimanjaro ina wanafunzi 1655 wasiojua kusoma , kuandika na kuhesabu kwa kipindi cha mwaka 2013/2014, wanafunzi hao ni wa kuanzia darasa la tatu hadi la saba.

No comments:

Post a Comment