Monday, June 9, 2014

AFARIKI baada ya kusukumwa na wananchi wa kijiji cha jirani mkoani Mtwara


MKAZI wa Kijiji cha Mwembetogwa kata ya Muungano Wilaya ya Mtwara vijijini,mkoani Mtwara  Mohamed Chumila amekutwa amefariki baada ya kusukumwa na mwanamke wa kijiji cha jirani alipoenda nyumbani kwake usiku
.

Afisa mtendaji wa kijiji hicho Nicolaus Mrope amesema mwili wa marehemu umekutwa ukiwa umeanguka nje ya nyumba ya mwanamke huyo na amekiri kumsukuma pasipo kujua  kama angekufa.

Mrope ameeleza kuwa mwanamke huyo amedai kuwa marehemu alifika nyumbani kwake saa nne usiku na kugonga mlango na alipofungua alikutana naye na kumtaka wafanye mapenzi na alipomkatalia ndipo wakaanza kuvutana.

Ameeleza kuwa baada ya kumsukuma alirudi ndani na kujifungia  akiamini mwanaume huyo angeamka na kurudi kwa mke wake, lakini alipoamka asubuhi alikuta umati wa watu nje ya nyumba yake wakishuhudia maiti ya Chumila.

Mwanamke huyo bado anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi.



No comments:

Post a Comment