Monday, June 9, 2014

WATUMISHI wa wizara ya maliasili watakiwa kushirikiana na wanavijiji vinavyozunguka hifadhi za Taifa


WIZARA ya Maliasili na Utalii imetakiwa kuangalia sheria za ujirani mwema na vijiji jiarani na hifadhi za taifa kwa kuhakikisha kuwa jamii inapata ushirikiano wa kutosha toka kwa wafanyakazi wa idara ya maliasili hasa askari wa maliasili.

  Changamoto hiyo imetolewa na wakazi wa vijiji vya Sanze na Mangula vilivyopo wilayani Kkilombero, mkoani Morogoro kufuatia baadhi ya  watumishi kutokuwa na ushirikiano mzuri na wananchi wa vijiji hivyo.

  Wakiongea na Mbiu ya maendeleo leo asubuhi katika kijiji cha Sanze wilayani humo, baadhi ya wananchi wamesema kuwa, ni kweli maliasili ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa hasa katika kuingiza pato Taifa lakini ni vyema wizara ikatambua kuwa kabla ya kuanzishwa kwa hifadhi hizo wananchi walikuwepo na wanahaki ya kutumia baadhi ya rasilimali kwa kupata maelezo toka kwa wakuu wa idara husika.

Wamesema , baadhi ya watendaji wa  maliasili hawana uhusiano mzuri na wanakijiji jambo ambalo linakwamisha uafanisi wa uendelezaji wa maliasili za Taifa kupitia misitu ya Hifadhi za Taifa na wanyama pori.
 Kufuatia hali hiyo wameiomba wizara ya maliasili kuwa na semina ,warsha na makongamano ya mara kwa  mara katika vijiji jirani na hifadhi za taifa kwa lengo la kutoa elimu kwa umma namna ya kutumia maliasili hizo sanjari na utii wa sheria na kanuni zilizowekwa na wizara ya maliasili.  










No comments:

Post a Comment