Monday, June 9, 2014

MAITI ya mtoto yaokotwa eneo la Mabibo external jijini DAR


MAITI ya mtoto   mchanga imeokotwa  ikiwa imevilingishwa  kwenye kanga na kuwekwa  kwenye mfuko wa rambo  imeokotwa ikiwa imetupwa  pembezoni mwa mto uliopo  mabibo External  jijini dares-salaam.


Mwili wa mtoto huyo  umegundulika  na muokota  chupa za plastiki  ambapo alitoa  taarifa polisi , ambapo  askari polisi  walifika eneo la tukio  na kukuta maiti hiyo.

Akizungumza na mbiu ya maendeleo, Askari wa jeshi la polisi , sajest  primi Joseph aliyeuchunguza mwili huo  amesema hilo ni tukio la tatu  mfululizo kutokea katika mto huo  na matukio  mengine ya aina hiyo  yamepishana mwezi mmoja .

Mashuhuda waliokuwa eneo la tukio wamelaani vikali kitendo hicho na kusema wanadamu wamekuwa hawana utu na hivyo  kufanya matendo ya kinyama  bila uoga .

Aidha wametoa lawama zaidi kwa madaktari  ambao wanawasaidia akina dada kutoa mimba    na kuwataka kuacha tabia hiyo


No comments:

Post a Comment