Sunday, June 8, 2014

WALEMAVU wilayani Kisarawe, mkoani Pwani waziomba Taasisi na mashirika kuwajengea msikiti



MWENYEKITI wa Jumuiya ya uchumi na maendeleo ya walemavu nchini(JUMAWATA) Bwana Mshamu Mzanda amezitaka Taasisi na mashirika ya watu binafsi nchini kujitokeza katika kijiji cha Mtamba wilayani Kisarawe kuwasaidia walemavu wa kiislamu kuwajengea msikiti kwaajili ya kufanya ibada.


Akiongea na Mbiu ya Maendeleo wilayani Kisarawe mkoani Pwani mapema leo, mwenyekiti huyo amesema kijiji cha Mtamba wilayani humo kina walemavu 324  wenye dini tofauti huku zaidi ya asilimia 50 ya walemavu hao wakiwa  ni waislamu lakini hawana nyumba ya ibada.

Amefafanua kuwa, wakristo wana kaniasa ambalo limejengwa kwa msaada wa Taasisi moja toka nchini Korea toka hali ambayo inawafanya wamuabudu mwenyezimungu katika mazingira mazuri kinyume na waislamu.

Amesema , wao hawahitaji fedha wananchihitaji kujenga msikiti kwaajili ya ibada kisha wakabidhiwe kiongozi wa dini na mwalimu kwaaajili ya kuwafundisha dini  watoto wa kiislamui  wa jamii ya walemavu.

JUMAWATA ina jumla ya ekari 450 iliyopewa na Halmashauri ya wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani mnamo mwaka 2007 kwaajili ya kuendesha shughuli za kilimo na ufugaji.  

No comments:

Post a Comment