Sunday, June 8, 2014

MGODI wa makaa ya mawe wilayani Rudewa unatarajiwa kuwa mkombozi wa kijamii na kiuchumi



IMEELZWA kuwa ujenzi wa Barabara ya Rudewa mpaka machimbo ya makaa ya m awe Mangaka ni mkombozi wa mabadiliko ya kiuchumi na kijamii wilayani Rudewa na mkoani Njombe kwa ujumla.


Wananchi wa vijiji vya Mlangali wilaya ya  Rudewa , mkoani Njombe wameeleza hayo mwishoni mwa wiki wakati wakiongea na mbiu ya maendeleo katika kueleza shukrani zao kwa serikali na wadau wa maendeleo waliofanikisha ujenzi wa barabara hiyo ambayo inatarajiwa kuwa mkombozi wa ajira kwa wananchi hao.

Wamesema kuwa  , kwa muda mrefu wilaya hiyo nyuma kimaendeleo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa muda mrefu wa miundo mbinu ya barabara inayounganisha wilaya  hiyo na mikoa ya Ruvuma, Mtwara na Iringa.

Hata hivyo wananchi hao wameiomba serikali kuhakikisha kuwa mgodi wa maka yam awe wilayani  humo unatoakipaumbele cha ajira kwa wazawa ili kuwasaidia kujikwamua kiuchumi kwa lengo la kuondokana na umaskini wa kipato.

No comments:

Post a Comment