Tuesday, June 17, 2014

DEREVA wa bodaboda afariki kwa ajali ya gari



 
Kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi kinondoni Camilius  Wambura akiongea na vyombo vya habari
DEREVA mmoja wa bodaboda aliyefahamika kwa jina la Ally Omary mwenye umri wa Miaka (29) amekufa katika ajali iliyotokea barabara ya new Bagamoyo baada ya kugongana na gari la kijeshi Lugalo.


Kamanda wa polisi wa Wilaya ya Kinondoni Camilius Wambura amesema tukio hilo limetokea hivi karibuni lango kuu la Lugalo jeshini barabara ya Bagamoyo Wilaya ya Kinondoni .

Amesema gari la kijeshi aina ya Iveco ambalo halikufahamika namba ya gari hilo na dereva wake ilitokea upande wa barabara ya Lugalo jeshini hospitali na kwenda upande wa pili kwa njia isiyoruhusiwa na kugongana na pikipiki hiyo. Pikipiki yenye ya usajili T956 BAH ambapo kwa mujibu wa Wambura dereva wa gari hilo la kijeshi ametoroka mara baada ya tukio hilo.

No comments:

Post a Comment