![]() |
| Mkuu wa wilaya ya Kilombero Hassan Masala |
MKUU wa
wilaya ya Kilombero,mkoani Morogoro Hassan Masala amewaagiza wazazi,wenyeviti
wa vijiji na viongozi wa serikali na sekta binafsi kuchangia chakula shuleni
zoezi litakalo anza kuanzia Julai.
Katika hotuba ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika iliyosomwa
na makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Iluminata Kapinga mjini
Ifakara mkuu huyo alisema mpango huo unalengo la kuokoa zaidi ya watoto 47,423
katika shule za msingi 102.
Hata hivyo alikerwa na tabia ya walimu kutoripoti wakiwemo walimu
208 kati yao 119 wanawake na 89 wanaume kati ya walimu wa sekondari 233
wakiwemo wanawake138 na wanaume 98 waliotakiwa kuripoti mwaka huu wilayani
humo.
Kuhusu umbali kutoka nyumbani hadi shuleni,mkuu huyo alisema mpango mkakati wa ujenzi hosteli umeanza ambapo hosteli nane zimejengwa na serikali na Mbili kujengwa na wazazi.
Akizungumzia hali ya vitabu alisema tayari serikali imefanikiwa kutoa hadi kufikia uwiano wa 1:1 nakuwa changamoto iliyobaki ni kwenye vitabu vya masomo ya sanaa ambayo itatatuliwa hivi punde.

No comments:
Post a Comment