Sunday, June 29, 2014

DIWANI atumia jina la mkuu wa wilaya kukusanya fedha kinyume cha sheria




Mkuu wa wilaya ya Kilosa Elias Tarimo
HATIMAE usemi wa za mwizi arobaini umemkumba Diwani wa kata ya Mabwerebwere wilayani Kilosa,akidaiwa kutumia jina na nafasi ya mkuu wa wilaya hiyo Elias Tarimo kujikusanyia mifugo na fedha kwa wapigakura wake kwa kisingizio cha kugharimia ugeni na hafla za kitaifa wilayani humo.


Diwani huyo Matei Kayanda(CCM)anadaiwa kunaswa karibuni baada ya kujitoma kwa mfugaji Teyani Maumbi mkazi wa kijiji cha Kondoa akimtaka ampe Ng’ombe wawili na shilingi 200,000 zitakazotumika kitoweo kwenye ugeni wa mbio za Mwenge uliodaiwa kupita wilayani humo Juni 22.

Mkuu wa wilaya hiyo Elias Tarimo amekili kuwepo kwa tukio hilo alilodai lililenga kumchafua nakuwa tayari mtuhumiwa alitengenezewa mtego uliomnasa na suala hilo lipo kwenye vyombo vya sheri likiandaliwa utaratibu wa kupelekewa mahakamani.
  
Aidha tarimo alisema binafsi amekuwa akikerwa na baadhi ya tabia ya viongozi kutumia jina na cheo chake kuwadanganya watu kulindwa endapo watatekeleza kutoa vitu wanavyoombwa na watu wasio na nia njema na yeye nakuwa anakusudia kuukomesha mtandao huo kwa kuwafikisha kwenye mamlaka za kisheria.

Akisimulia mkasa huo Mfugaji Maumbi alisema siku ya tukio majira ya asubuhi kuelekea mchana Diwani huyo aliyemgeuza kitegauchumi chake kwa muda mrefu, alifika nyumbani kwake na kumweleza serikali ya wilaya imekaa na Mkuu wa wilaya hiyo amemwagiza kufika nyumbani kwa mfugaji kutaka ng’ombe hao na kiasi hicho cha fedha

Alimtaka haraka afike ofini kwake na alipofika alikuta safu yote ya utawala akiwemo kamanda wa Takukuru,Usalama wa Taifa, mkuu wapolisi OCD wilayni humo wakiwa ofisini ambao waliunda mtego uliofanisha kunaswa kwa diwani huyo.

Juhudi za kumpata diwani huyo Matei Kayanda kutoa ufafanuzi wa madai hayo zinaendelea licha ya kushindikana baada ya kuizima simu yake ya kiganjani(0786088870) alipotajiwa anyeeongea nae ni mwandishi wa habari.

Hata hivyo jeshi la polisi kupitia kaimu kamnda wake wa polisi John Laswai limekanusha kuwepo kwa tukio hilo ingawa aliahidi kuendelea kufuatilia kwa OCD wilayani Kilosa.

No comments:

Post a Comment