Sunday, June 29, 2014

UMOJA wa vijana waandaa kongamano la katiba




Wajumbe wa bunge la katiba
UMOJAwa Vijana wilayani Kilosa mkoani Morogoro unaandaa kongamano huru ili kuweza kuhamasisha kupata  katiba bora itakayokuwa na tija kwa Taifa kwa ujumla.


Hayo yameelezwa  juni 27 mwaka huu na Rais wa Umoja huo Denis Nyiraha katika mbiu ya maendeleo ambapo amesema wameamua kuanzisha umoja huo ili kuweza kufikisha kwa watu wote kuwa na uelewa juu ya suala zima la katiba.

Nyiraha amesema kuwa kongamano hilo linatarajia kufanyika hivi karibuni ili kuweza kutoa fulsa kwa wananchi kutoa maoni yao lakini pia kuweza kurudisha Uzalendo wa Taifa la Tanzania kwa ujumla.

Aidha Nyiraha ametoa wito kwa jamii kuweza kushiriki katika mchakato huo ili kusaidia kurejesha jitihada za uzalendo wa Mtanzania lakini pia kufanikisha kupata katiba bora ambayo itakuwa ni ya miaka hamsini ijayo.
Naye aliyejitambulisha kwa jina la Charles Golaga ameupongeza mfumo huo na kusema kuwa ni mzuri kwani una manufaa katika jamii ya lakini ameweza kuwashauri wanachama hao kuweza kuepuka siasa na badala yake uwajibikaji uwepo.


No comments:

Post a Comment