Friday, June 27, 2014

RAIS Rouhan awataka viongozi waislamu wautangaze mwezi wa RamadhanI



Rais Hassan Rouhan wa Iran akiongea na vyombo  vya habari

RAIS Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewatumia salamu za pongezi viongozi wa nchi zote za Kiislamu duniani kwa munasaba wa kuwadia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ambapo amewataka wautangaze mwezi wa Ramadhani mwaka huu kuwa ni 'Ramadhani ya Amani na Rahma'.


Aidha amewataka viongozi wa nchi za Kiislamu kujitahidi kuleta umoja na udugu miongoni mwa Waislamu kote duniani.

Katika ujumbe wake huo, Rais Rouhani amesema Ramadhani ni mwezi wa saumu, kiyamu na rehma na ibada na hivyo viongozi wa Kiislamu wanapaswa kuchukua hatua za kuimarisha umoja wa Kiislamu.
 Katika sehemu ya ujumbe wake, Dkt. Rouhani ameseama: 'Mwaka huu, Waislamu wanaukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani huku machafuko na misimamo mikali ikiusukuma ulimwengu wa Kiislamu katika hofu, ujahili, na ghadhabu mambo ambayo yanawaandalia maadui njia ya kutekeleza njama zao za jadi za kuwafarakanisha Waislamu sambamba na kuibua vita vya kimadhehebu na kikaumu."

No comments:

Post a Comment