Friday, June 27, 2014

WAZEE ,Korea kusini wajihusisha na biashara ya ukahaba




WAZEE  katika baadhi ya nchi huheshimika na kuwa akiba ya busara kwa kizazi cha vijana na zaidi ya yote huangaliwa na kusaidiwa kimaisha.


Huko nchini Korea Kusini maisha kwa wazee ambao walichangia katika uchumi wa Taifa hilo na ustawi wa taifa hivi sasa wanaishi katika mazingira magumu hali ambayo kwa wanawake wazee inawalazimu kubuni mbinu mpya za maisha kwa kujitumbukiza katika biashara haramu ya ngono kwa kuuza miili yao ili waweze kujipatia fedha za kuendesha maisha yao ya kila siku.
Taarifa hizo zinajuza kuwa, katika nchi zilizo nyingi na hata Afrika mashariki biashara ya ngono hufanywa na wasichana wadogo na hata wa umri wa kati kwa lengo la kujipatia kipato .
Akiwa amevalia koti lake jekundu,na kupaka rangi ya mdomo kwa ustadi Bi. Kim Uen Ja mwenye umri wa miaka 71 mavazi yake yanabainisha wazi kwamba angependa kuwa na muonekano wa msichana mdogo na mrembo, yupo katika eneo la kupumnzika la Jongno-3 subway station huku pembeni mwake akiwa na begi kubwa lililosheheni chupa ndani yake.
Bi. Kim ni mmoja kati ya wanawake wazee wa Korea ya kusini ambao hupendelewa kuuza kinywaji ambacho wanaume wanasema kinawaongezea nguvu kijulikanacho kwa jina la Bacchus, lakini wanawake hawa wanaouza vinywaji hivi baadhi yao ni wale wenye malengo ya kujiuza ili wapate fedha za kuendeshea maisha yao.









No comments:

Post a Comment