Friday, June 6, 2014

MAADHIMISHO ya siku ya mazingira duniani wilayani Kilosa yafanyika katika tarafa ya Magole


MAADHIMISHO ya siku ya mazingira Wilayani Kilosa yamefanyika hapoa jana  katika tarafa ya Magole kijiji cha Mbigiri Wilayani Kilosa, mkoani Morogoro.

Hayo yameelezwa na kaimu afisa na mazingira Brayson Shoo ofisini kwake alipokuwa akiongea na mbiu ya maendeleo ambapo amesema kuwa sababu hasa ya kufanyia maadhimisho hayo tarafa hiyo ni kutokana na janga la mafuriko lililotokea hivi karibuni tarafani humo ili wananchi waweze kujifunza jinsi ya kutunza mazingira.

Pia amesema kazi za usafi wa mazingira zimeanza huko Magole ikiwa ni pamoja na kupulizia dawa ya kuua wadudu kama mbu na wengineo kwenye kambi za wahanga na zinafanyika .

Aidha Shoo amesema kuwa mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa na kuwa kauli mbiu ya mwaka huu ni “TUNZA MAZINGIRA ILI KUKABILIANA NA MABADILIKOYA TABIA YA NCHI”.

No comments:

Post a Comment