Friday, June 6, 2014

UWT mkoani Morogoro watakiwa kutokata tamaa katika kujikwamua kiuchumi


WANAWAKE Mkoani Morogoro wametakiwa kutokata tamaa katika shughuli za kiuchumi ili kuondokana na utegemezi pia ombaomba kwa wanaume zao na jamii.

 Ushauri huo umetolewa na mwenyekiti wa umoja wa wanawake mkoa wa Morogoro Mariam Kyamani kwenye sherehe ya miaka 10 ya kikundi cha kijamii cha Upendo Women Group  kilichopo kata na mtaa wa Tubuyu manispa ya Morogoro.


Kyamani ambaye pia ni diwani wa kata ya Kingolwila alisema dhana ya mwanamke kuendelea kuwa tegemezi imepitwa na wakati badala yake wanatakiwa kujishugulisha kulimngana na flsa walizonazo.

Katika risala ya kikundi hicho pamoja na mambo mengine iliomba mashirika na taasisi mbalimbali kuendelea kusaidia vikudi vya kijamii kwa ajili ya kuleta mabadiliko ya kinamama ya kiuchumi.


No comments:

Post a Comment