Friday, June 6, 2014

HOSPITALI ya St Francis ya Ifakara yakabidhiwa gari la kubeba wagonjwa lenye thamani ya shilingi milioni 6.8


CHAMA cha madaktari rafiki wa Ifakara,mkoani Morogoro  kwa kushirikiana na shirika la MIVA toka nchini Austaria wameikabidhi hospitali ya rufaa ya Mt.Francis gari la kubebea wagonjwa lenye thamani ya shilingi milioni 61.8.


Makabidhiano ya gari hilo aina ya Landcriser yamefanyika jana katika hospitali hiyo mbele ya uongozi wa hospitali hiyo chini ya  askofu wa jimbo la Ifakara Mhashamu Salitaris Libena na Rais wa Chama cha madaktari rafiki wa Ifakara Dr Willi Schennach na wafanyakazi wa hospitali hiyo.

Mkurugenzi wa hospitali hiyo Dk Angelo Nyamtema alisema kuwa chama hicho cha madaktari rafiki wa Ifakara kimeanza kuisaidia hospitali hiyo kwa miaka 20 sasa kwa kuwapatia vifaa mbalimbali ikiwemo jenereta,mashine za kufulia,vifaa tiba,fedha na kusomesha madaktari bingwa katika hospitali hiyo na pia kuleta madaktari bingwa kutoka nchini mwao kuja kubadilishana utaalamu na madaktari wa hospitali hiyo.

Dk Nyamtema alisema msaada wagari hilo umekuja wakati muafaka kwani gari la mwanzo halikuwa na vifaa muhimu ila la sasa limekamilika na litasaidia kwa wagonjwa mahututi kuwapelekea katika hospitali nyingine kubwa kama ikitokea dharura.

Alisema kuwa hospitali yoyote inayotoa huduma bora lazima iwe na gari la uhakika la wagonjwa hivyo kuwaahidi wafadhili hao kuwa gari hilo jipya walilopewa watalitumia kwa malengo yaliyokusudiwa na sio katika shughuli nyingine.

Kwa upande wake askofu wa jimbo la Ifakara Mhashamu Libena  alisema mchango wa gari la wagonjwa ni habari njema si tu kwa hospitali bali pia kwa jamii katika huduma pana zaidi ambapo huduma hii itaokoa maisha kwa wagonjwa wengi hivyo kuwapongeza wafadhili hao wawili kwa ukarimu wao na kuwaomba kuendelea kuwasaidia kama walivyoanza tokea  miaka 20 iliyopita.


No comments:

Post a Comment