Friday, June 6, 2014

MACHINJIO 20 kati ya 900 yaliyopo nchini ndiyo yana usajili


MAMLAKA  ya chakula na Dawa (TFDA) imesema kati ya machinjio zaidi ya 900 yaliyopo nchini ni 20 pekee yamesajiliwa jambo ambalo linalochangia uwepo wa huduma mbovu zisizozingatia viwango vinavyotakiwa.

Hayo yamesemwa ivi karibuni jijini Dar es salaam na Kaimu Mkurugenzi wa TFDA Raymond Wigenge wakati akizungumza na mbiu ya maendeleo mara baada ya kufungua semina ya siku mbili kwa wajasiriamali wadogo wa vyakula kutoka mikoa mbalimbali nchini.


  Wigenge aliyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu katika ufunguzi wa semina hiyo amesema TFDA inatambua changamoto zinazoikabili sekta ya nyama , ikiwemo uchafu na miundimbinu katika machinjio na imejiandaa kuweka mikakati mipya kupambana na hali hiyo.
  Amesema TFDA imetoa agizo la maboresho zaidi ya miaka mitatu iliyopita na sasa inaandaa mikakati kuleta mapinduzi katika sekta ya nyama hasa machinjio ili kuboresha huduma , afya ya jamii na kuhakikisha sheria na miongozoinazingatiwa.


No comments:

Post a Comment