Saturday, June 7, 2014

WANANCHI wilayani Kilosa waaswa kutunza mazingira



WANANCHI Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro , wametakiwa kuacha kutupa taka nje ya Dampo zilizojengwa kwa ajili ya kutupa taka hizo kwani ni hatari na inweza  kuleta milipuko ya magonjwa.
Hayo yameelezwa na kaimu Afisa Usafi Wilaya ya KIlosa MUHAMMADI MUHOMBORAGE hivi karibuni ofisi kwake  wakati akiongea na Mbiu ya Maendeleo ambapo amesema kuwa kuna Baadhi ya wafanya Biashara hutupa uchafu  nje ya dampo maarufu kwa jina Vizimba wakati wa usiku na kusababisha taka hizo kuzagaa hovyo.


Aidha Muhomedi Muhomborage akiongea suala la wanaotupa taka nje ya vizimba nyakati za usiku amesema umewekwa mkakati kuweza kuwabaini na kuwakamata watu hao na ambapo hatua kali zita chukuliwa dhidi  yao.

Ameongeza kusema kuwa mtu yoyote atakaekamatwa akitupa ovyo taka nje ya kizimba hatozwa faini papohapo na kufikishwa mahakamani.

   

No comments:

Post a Comment