JESHI la polisi
Wilaya Kilosa Mkoani Morogoro limetoa wito kwa wafanyabiashara wenye MADUKA
MAKUBWA kufunga mapema maduka yao ili kuepusha kuvamiwa na majambazi .
Wito
huo umetolewa mapema jana na Mkuu wa Polisi (OCD) Wilaya ya kilosa BREKI MAGESA wakati akizungumza na Mbiu ya
Maendeleo ofisini kwake.
OCD
MAGESA amesema kuwa kwa hali ya sasa hali si shwari kwenye jamii ambayo
imechanganyika na watu wabaya ambao wamekuwa wanafanya uhalifu usiku kwa
kuvamia kwenye maduka na kupora fedha na vitu mbalimbali .
Amesema
kuwa wanapaswa wafunge maduka yao angalau ifikapo saa moja jioni kukiwa
kweupe bado na mwanga ili kuepusha vivutio vya waarifu kwani
kufunga maduka yao usiku giza limeingia husababisha kumpa mwanya muharifu
kuvamia na hata kumtambua muharifu huyo inakua ngumu kutokana na giza.
Mapema
hivi karibuni majambazi yakiwa na siraha yalivamia maduka usiku wa saa tatu
maeneo ya Kimamba na kupora fedha na simu kwa wafanya biashara wenye maduka.
No comments:
Post a Comment