Saturday, June 7, 2014

SERIKALI yaombwa kujenga uzio wa hospitali ya wilaya ili kuepusha utupwaji taka ovyo



SERIKALI imeombwa kujenga uzio wa tofari katika hospitali ya wilaya yaKilosa, mkoani Morogoro,ili kuepusha uchafuzi wa mazingira kutokana na tabia ya baadhi ya wananchi wanaotupa taka kando kando ya hospitali hiyo.


Ombi hilo limetolewa  hivi karibuni na Afisa Afya wa wilaya ya Kilosa  Bi Rose Nguruwe   wakati wa wiki ya kuadhimisho siku ya mazingira duniani.

Amesema hospitali ya wilaya inakabiliwa  na changamoto ya wananchi kutupataka  ovyo katika eneo la jirani na hospittali hali inayohatarisha afya ya wananchi nawagonjwa waliopo katika eneo hilo.

Hata hivyo Bi Rose amelipongeza jeshi la magereza wilayani humo kwa kushiriki kikamilifu katika maadhimisho ya wiki mazingira kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya hospitali ya wilaya.

No comments:

Post a Comment