Saturday, June 7, 2014

WAKULIMA wa ao la Muhogo Mtwara waipongeza taasisi ya IIITA



WAKULIMA  wa zao la muhogo mkoani Mtwara, wameipongeza Taasisi ya kimataifa ya utafiti na uendelezaji wa zao la muhogo (IITA)kwa jitihada zake za kuwasaidia wakulima wa zao hilo mkoani humo.


Wakiongea na mbiu ya maendeleo mapema leo , wakulima hao wameeleza kuwa Taasisi hiyo ifanya kazi kubwa ya kuchangia maendeleo ya wakulima wa muhogo ikiwa nipamoja nakutoa elimu ya namana ya kupambana na magonjwa na wadudu waharibifu wa zao hilo, utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na muhogo na elimu ya namna ya kutatauta masoko ya bidhaa hizo.

Taasisi ya International Institute of Tropical Agriculture(IITA) iliyopo Mikocheni jijini Dar es salaam inatoa mchango mkubwa wa kukuza zao la muhog kwa kufanya tafiti na kuiwaezesha wakulima wa zao hilo katika mikoa mbalimbali hapa nchini ukiwemo mkoa wa Mtwara.

Mkoa wa Mtwara ni miongoni mwa mikoa iliyopo katika mpango maalum  wa Taasisi hiyo wa kuwaezesha wakulima wa zao la muhogo  kupambana na umaskini wa kipato. 

No comments:

Post a Comment