![]() |
| Wakulima wakiuza mazao sokoni |
WITO umetolewa
kwa Serikali kupanga bei maalumu kwa wakulima itakayo weza kuleta tija pindi
watakapo vuna mazao yao hali itakayo pelekea kuepukana na bei za wafanya
biashara ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Wito huo umetolewamapema jana na wananchi wa wilayani kilosa,mkoani
Morogoro wakati wakiongea katika kikao walichokaa na waandishi wa habari
kujadili mada iliyokuwa ikisema ni kipaumbele gani kimetolewa kwa wakulima juu
ya mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN).
Mmoja wa wananchi hao kutoka Mgeta,iwlayani
Mvomero ambaye hatukuweza kupata jina
lake amesema kuwa bei wanayouzia mazao yao inapangwa na wafanya
biashara kwani bei zao haziendani na gharama za uzalishaji hivyo
kushindwa kuendesha maisha yao na kubaki kuwa watu wa maisha duni.
Mwananchi huyo amefafa kuwa Serikali
inatakiwa kuweka mikakati ya bei ya mazao
ya wakulima kama ilivyo kwa wafanya biashara ili waweze kuepukana
na umasikini kupitia kilimo.

No comments:
Post a Comment