![]() | |
| Mkurugenzi wa Twaweza Rakhesh Rajan akiongea na vijana |
TUO cha msaada wa saidizi wa Kisheria Paralegal (KIPA)
kilichopo Kilosa Mkoani Morogoro kimepokea vitabu vya aina 3 vya usaidizi wa
kisheria kutoka Kituo cha Sheria na haki za Binadamu kwa kushirikiana na
Twaweza lengo ni kuwaongezea uwezo wa kujitambua wananchi kuhusiana na Katiba
mpya na haki zao.
Akizungumza na mbiu ya maendeleo
ofisini kwake Msaidizi wa Kisheria wa Wilaya ya Kilosa Vimwaya Manyoli amesema
kuwa wamepokea jumla ya vitabu elfu ishirini na nne juni 22 mwaka huu ambavyo
ni kitabu Katiba ni nini,Twende wapi na Hashuki mtu hapa.
Amesema kuwa vitabu hivyo ni
vizuri kwani vinaelimisha Jamii na wananchi kwa Ujumla pia mtu anaweza kuelewa
kwa kuangalia picha zilizomo kitabuni humo na amewashauri wananchi kuwa
na mazoea ya kujisomea vitabu ili waweze kukuza uelewa wao wa Kimawazo.
Aidha ameongeza kuwa wananchi endapo
watajenga mazoea na kusema kuwa yaliyomo ndani ya vitabu hivyo yanasadifu
maisha yaliyopo sasa.

No comments:
Post a Comment