Wednesday, June 25, 2014

ZAIDI ya asilimia 62 ya watoto Manispaa ya Morogoro wamefanyiwa ukatili.


Mkuu wa wilaya ya Morogoro Saidi Amanzi akiongea na waandishi wa habari

UTAFITI wa ukatili na unyanyasaji kwa wanawake na watoto uliofanywa hivi karibuni na Taasisi ya Tanzania Women Health Network TWHN Manispaa ya Morogoro umebaini zaidi ya asilimia 62 ya watoto katika manispaa hiyo wamefanyiwa ukatili Kisaikolojia,Jinsia na kimwili na watu wa karibu wakiwemo ndugu na jamaa.


Hayo yamo kwenye taarifa fupi ya uzinduzi wa Taasisi hiyo  iliyosomwa na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo nchini Gloria Kasilo kwa Mkuu wa wilaya ya Morogoro Said Amanzi aliyewakilishwa na Afisa elimu Taaluma Manispaa hiyo Christopher  Wangwe.

Mbali na utafiti huo Mkurugenzi Gloria alisema Taasisi hiyo inayopambana na ukatili kwa mama na mtoto unakua kila siku ambapo takwimu za kimataifa za 2011 zinaonyesha kati ya watoto 10 wa kike sita wamefanyiwa ukatili huo majumbani,shuleni na mitaani ambapo kupitia taasisi hiyo kati ya 10,saba wamefanyiwa uakatili.

Alisema lengo la Taasisi hiyo ni kumwezesha mwanamke hasa mtoto wa kike kujikomboa kwa kupata elimu itakayomwezesha kuzikabili changamoto zinazowakabili katika mazingira walipo,aweze kujisimamia na kumtoa kwenye utegemezi na kujiletea  maendeleo.
   

No comments:

Post a Comment